Jorge Mario Bergoglio achaguliwa Papa mpya

Baba Mtakatifu mpya Jorge Bergoglio akitokea kwa mara ya kwanza Vatican Mar 13, 2013. (Vatican TV)

Vatican imemchagua Kadinali Jorge Mario Bergoglio kuwa Baba Mtakatifu mpya kuongoza kanisa katoliki. Bergoglio kutoka Argentina atakuwa baba mtakatifu wa kwanza kutoka Amerika Kusini katika historia ya kanisa katoliki.