Katibu Mkuu wa NATO anasema mlipuko karibu na mpaka wa Ukraine huenda ulisababishwa na kombora la Ukraine lililofyatuliwa dhidi ya Russia

Your browser doesn’t support HTML5

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Brussels baada ya mkutano wa Baraza la Atlantiki Kaskazini, Katibu Mkuu wa NATO, Jens Stoltenberg anasema washirika wote wa NATO walikubaliana na tathmini hiyo ambayo ilitokana na uchunguzi wa awali na kwamba uchunguzi zaidi unaendelea.