Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaonya juu ya njaa nchini Somalia na kuongezeka kwa vifo vya watoto katika Pembe ya Afrika

Your browser doesn’t support HTML5

Pembe ya Afrika inashuhudia mwaka wake wa nne mfululizo kwa kushindwa kupata mvua tukio la hali ya hewa ambalo halijaonekana kwa angalau miaka 40. Kama ukame utaendelea shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) linaonya kwamba watu milioni 20 watakabiliwa na njaa kali mwishoni mwa 2022