Mgandamizo wa hewa katika kusini mashariki mwa bara la Afrika ndio sababu ya upepo mkali

Your browser doesn’t support HTML5

Wakati msimu wa mvua za Vuli ukiripotiwa kuchelewa katika maeneo mengi nchini Tanzania, taarifa toka mamlaka ya hali ya hewa nchini humo imeeleza kuwa kuimarika kwa mfumo wa mgandamizo wa hewa katika maeneo ya kusini mashariki mwa bara la Afrika ndio sababu ya upepo mkali katika maeneo ya bahari ya hindi hali ambayo imeonekana kwa takriban siku tatu na kusababisha kusitishwa kwa huduma za usafiri kwenda visiwani Zanzibar.