Ulinzi waimarishwa ufunguzi Kombe la Dunia 2018

Nembo rasmi ya Kombe la Dunia 2018

Ulinzi mkali umeimarishwa katika uwanja wa Luzhniki, mjini Moscow nchini Russia ambapo kutafanyika ufunguzi wa Kombe la Dunia Russia 2018 muda mchache ujao.

Mashabiki tayari wameshajisogeza uwanjani hapo kushihudia ghafla ya ufunguzi itakayofuatiwa na mchezo baina ya wenyeji Russia na Saudi Arabia.

Your browser doesn’t support HTML5

Russia 2018 kabla ya mechi ya ufunguzi

Russia imepeleka maelfu ya polisi katika miji yote 11 itakayokuwa mwenyueji wa mashindano hayo yatakayo chukuwa mwezi mmoja.

Serekali ya Russia ipo makini kutokana na kumbukumbu ya tukio la kigaidi lililofanyika mjini Marseille nchini Ufaransa mwaka 2016, katika mchezo wa mashindano ya Ulaya.