Marubani wa Kenya Airways warudi kazini

Ndege ya Kenya Airways

Marubani wa shirika la ndege la Kenya Airways wanatarajiwa kurudi kazini siku ya Ijuma baada ya kufikia makubaliano na wakuu wa shirika hilo juu ya madai yao ya kufukuzwa mkuu wa shirika lao.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kenya Airways Bi.Wanjiku Mugo, ameiambia Sauti ya Amerika kwamba ingawa hawezi kuthibitisha tunapozungumaza, lakini wamepata habari kweamba marubani watarudi kazini kuanzia Ijuma asubuhi, lakini wanasubiri kupatqa taarifa rasmi kutoka chama chao cha marubani Kenya KALPA.

Your browser doesn’t support HTML5

Mahojiano na Wanjiku Mugo wa Kenya Airways

Marubani wanadai kufukuzwa kwa Mkurugenzi Mkuu wa Kenya Airways Mbuvi Ngunze kutokana na mpango wake wa kufanya marekebisho ili kuokoa shirika hilo linalokumbwa na matatizo ya kifedha.

Katibu Mkuu wa KALPA Paul Gichinga ameiambia Sauti ya Amerika kwamba hawawezi kueleza makubaliano yaliyofikiwa bado lakini wameridhika kutokana na kwamba wakuu wa shirika hilo wamekubaliana na baadhi ya madai yao.