Zaidi ya watu 50 wauwawa mkoa wa Pwani Kenya

Wanajeshi wa Kenya wakijiandaa kupanda lori kuelekea Liboi, Kenya karibu na mpaka na Somalia

Mauaji hayo yilitokea wakati watu wenye silaha kutoka jamii ya Pokomo waliposhambulia kijiji kimoja katika eneo la Reketa.

Kufuatana na mwenyekiti wa baraza la utawala la wilaya ya Mto Tana Diwani Salim Ngolo ni kwamba "leo si siku ya huzini mkubwa kabisa kwa sababu watu wasio na hatia waliweza kumalizwa nma kundi haramu. Kufuatana na watu wangu katika mji wa Reketa watu 68 waliuwawa."

Your browser doesn’t support HTML5

zaidi ya watu 50 wauwawa Tana River


Anasema kundi la watu lilivamia nyumba za watu wakati wa usiku na kutia moto, na kuwashambulia kwa mapanga wale walojaribu kujinusuru.
Polisi wa mkoa wa Pwani wanasema idadi ya walofariki ni watu 48 wengi wao wanawake na watoto.