Serikali ya Kenya inamiliki asilimia 48.9 ya hisa za shirika hilo ambalo limekuwa likipata hasara kila mwaka wa kifedha. Wabunge hata hivyo wametofautiana kuhusu jinsi ya kulipa madeni ya KQ, baadhi wakisema wananchi walipa kodi hawastahili kugharamia makosa ya usimamizi yaliyofanywa na watu binafsi