Ndege ya jeshi la Iran ya mizigo Boeing 707 ambayo ilikuwa imebeba nyama kutoka Kyrgyzstan imeanguka Jumatatu ilipokuwa inajaribu kutuwa magharibi mwa mji mkuu wa Iran, na watu 15 walio kuwa ndani yake wamepoteza maisha na mtu mmoja tu ndiye aliye salimika, vyombo vya serikali vimesema.