Trump hata hivyo alisema kufuatia hatua yake ya kutangaza Dharura ya Kitaifa, anatarajia upinzani mkubwa mahakamani lakini akasema yupo tayari kuitetea kutoka mahakama ya chini hadi ya juu akieleza imani kwamba mwishowe, atapata pesa anazotaka kwa ujenzi wa ukuta huo.