Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Juni 03, 2023 Local time: 07:12

Mkenya avunja rekodi ya dunia ya mbiyo za Marathon


Dennis Kimetto mwanaridha kutoka Kenya amevunja rekodi za mbiyo za Marathon mjini Berlin, Ujerumani siku ya Juampili na kuwa mtu wa kwanza kukimbia mbiyo hizo kwa chini ya saa 2 na dakika tatu.

Kimetto mwenye umri wa miaka 30, alimpita Mkenya mwenzake bingwa wa mbiyo hizo Emmanuel Mutai, karibu mili tatu kabla ya kumaliza mbiyo na kuweka rikodi ya saa 2 dakika 2 sekunde 27.

Rikodi ya awali ilikua imewekwa na Mkenya mwenzake Wilson Kiplagat mwaka mmoja uliyopita huko huko Berlin, alipokimbia muda wa saa 2:03:23. Katika mbio za Jumapili Mkenya Mutai alishika nafasi ya pili akitumia mjda wa saa 2:03:13 akifuatwa na Methopia Abera Kuma aliyetumia saa 2:05:56.

Kwa upande wa wanawake Methopia Tirfi Tsegaye alinyakua ushindi akitumia muda wa 2:20:18, huku mwenzake Feyse Tadese alishika nafasi ya pili akitumia muda wa 2:20:27

XS
SM
MD
LG