Mahakama ya Kikatiba ya Madagascar siku ya Ijumaa ilimtangaza Rais aliye madarakani Andry Rajoelina kuwa mshindi wa uchaguzi wa mwezi uliopita, na hivyo kumpa muhula mwingine wa tatu.
Rajoelina alipata asilimia 58.96 ya kura zilizopigwa, mahakama ilisema baada ya kutupilia mbali changamoto mbalimbali zilizowasilishwa dhidi ya matokeo ya awali yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi.
Andry Rajoelina amechaguliwa kuwa rais wa jamhuri ya Madagascar na anachukua madaraka yake punde tu atakapoapishwa, alisema Florent Rakotoa-risoa, mkuu wa mahakama ya kikatiba.
Mojawapo ya changamoto ambazo zilitupiliwa mbali ni pamoja na moja kutoka kwa mshindi wa pili, mbunge Siteny Randriana-soloniaiko, ambaye alipata asilimia 14.39 ya kura kwa mujibu wa mahakama.
Forum