Bingwa mtetezi wa Olimpiki na nyota anayeshikilia rekodi ya dunia, Eliud Kipchoge wa Kenya ameshinda mbio za marathon zilizofanyika huko Twente Airport mjini Enschede, Uholanzi Jumapili.
Katika mashindano hayo Katharina Steinruck wa Ujerumani alikuwa wa kwanza kuvuka mstari katika mbio za wanawake. Mbio hizi ni sehemu ya kupasha misuli moto tayari kwa michezo ya Olimpiki ya Tokyo.