Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Februari 11, 2025 Local time: 04:53

Kamati Kuu ya Kitaifa ya ANC yataka hali ya dharura kitaifa kutangazwa


Rais wa Baraza la Kitaifa la Kitaifa la Afrika Cyril Ramaphosa atoa salamu za nguvu nyeusi mwishoni mwa Mkutano wa 55 wa Kitaifa huko Johannesburg, Afrika Kusini, Jumanne, Desemba 20, 2022
Rais wa Baraza la Kitaifa la Kitaifa la Afrika Cyril Ramaphosa atoa salamu za nguvu nyeusi mwishoni mwa Mkutano wa 55 wa Kitaifa huko Johannesburg, Afrika Kusini, Jumanne, Desemba 20, 2022

Kamati Kuu ya Kitaifa ya chama tawala cha African National Congress (ANC) nchini Afrika Kusini inataka hali ya dharura ya kitaifa kutangazwa sawa na ile iliyotangazwa kukabiliana na janga la Covid 19  ili kusaidia kumaliza hali ya ukosefu wa umeme.

Kamati Kuu ya Kitaifa ya chama tawala cha African National Congress (ANC) nchini Afrika Kusini inataka hali ya dharura ya kitaifa kutangazwa sawa na ile iliyotangazwa kukabiliana na janga la Covid 19 ili kusaidia kumaliza hali ya ukosefu wa umeme.

Katibu Mkuu wa ANC Fikile Mbalula aliwaambia waandishi wa habari leo Jumanne kwamba kamati kuu ya utendaji ya ANC baada ya kukutana imeitaka kamati ya kukabiliana na mzozo wa nishati inayomshauri Rais Cyril Ramaphosa kuharakisha kazi yake.

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ambae hakuhudhuria mkutano wa Jopo la Kiuchumi Duniani huko Davos mwezi huu kwa sababu ya ukosefu wa umeme, anatarajiwa kutangaza hatua mpya za kuongeza huduma za umeme wakati wa hotuba yake juu ya hali ya taifa hapo Februari 9.

XS
SM
MD
LG