Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Februari 11, 2025 Local time: 00:55

Iran inasema itaendelea na juhudi za kuachiliwa kwa afisa wake wa zamani


 Hamid Noury (L) akiwa na wakili wake Thomas Soderqvist wakati akisomewa mashtaka mjini Stockholm huko Sweden. Nov. 23, 2021.
Hamid Noury (L) akiwa na wakili wake Thomas Soderqvist wakati akisomewa mashtaka mjini Stockholm huko Sweden. Nov. 23, 2021.

“Uamuzi huu usio wa haki na wa kukasirisha  haumalizi juhudi za kidiplomasia za Iran za kumrejesha na kumuachia huru raia huyu wa Iran", kulingana na msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Iran

Iran imesema itaendelea na juhudi za kutaka kuachiliwa huru kwa afisa wa zamani wa Iran aliyehukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kushiriki katika mauaji ya wafungwa wa kisiasa nchini Iran.

“Uamuzi huu usio wa haki na wa kukasirisha haumalizi juhudi za kidiplomasia za Iran za kumrejesha na kumuachia huru raia huyu wa Iran, na tutatumia njia zote za kisheria na zilizopo”, msemaji wa wizara ya mambo ya nje Nasser Kanaani alisema, bila ya kufafanua.

Jumanne iliyopita, mahakama ya rufaa ya Sweden iliidhinisha hukumu ya kukutwa na hatia pamoja na kifungo cha maisha kwa mauaji na uhalifu mkubwa dhidi ya sheria ya kimataifa kwa afisa wa zamani Hamid Noury.

Chumba cha mahakama ya Stockholm ikisikiliza kesi ya Hamid Nouri ambaye ni raia wa Iran
Chumba cha mahakama ya Stockholm ikisikiliza kesi ya Hamid Nouri ambaye ni raia wa Iran

“Tunapinga vikali hukumu hiyo na kile kilichotokea wakati wa kipindi kirefu cha raia huyu kizuizini, na haki zake za msingi hazijaheshimiwa katika magereza ya Sweden”, Kanaani aliuambia mkutano wa waandishi wa habari wa kila wiki. “Tunatumaini Sweden itachukua hatua kali kufidia makosa yake”.

Mapema mwezi Disemba, Iran ilianza kesi ya raia mmoja wa Sweden, Johan Floderus, aliyeajiriwa na Umoja wa Ulaya ambaye anashtakiwa kwa kuipeleleza Israel na “ufisadi duniani”, uhalifu ambao unapatiwa adhabu ya kifo.

Forum

XS
SM
MD
LG