Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 00:16

Chelsea na Benfica waripotiwa kukwaruzana juu ya Enzo Fernandes


Wachezaji wa Chelsea's Hakim Ziyech, Marc Cucurella na Enzo Fernandez wakati wakipasha misuli moto. Reuters
Wachezaji wa Chelsea's Hakim Ziyech, Marc Cucurella na Enzo Fernandez wakati wakipasha misuli moto. Reuters

Na wakuu wa timu za Chelsea na Benfica nusura wapigane kuhusu mustakbali wa Enzo Fernandez, kulingana na ripoti za kustusha nchini Ureno.

Mshindi huyo wa Kombe la Dunia wa Argentina alihamia Stamford Bridge kwa ada iliyoweka rekodi ya Uingereza yenye thamani ya pauni milioni 107 katika siku ya mwisho.

Pande zote mbili zilikuwa zimekwama katika mazungumzo tangu Kombe la Dunia, huku Chelsea wakimfanya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 kuwa mlengwa wao mkuu baada ya kufurahishwa na uchezaji wake nchini Qatar.

Mazungumzo kuhusu hatua hiyo ambayo yaliendelea kwa muda mrefu wa Januari na Jarida moja la Ureno sasa limefichua mvutano mkubwa kati ya kambi hizo mbili zilipokutana kuzungumza kuhusu Fernandez na jinsi Benfica walivyoshinikiza kwa Mateo Kovacic kujumuishwa katika mpango wa kubadilishana.

Hata hivyo The Blues -Chelsea inakanusha taarifa hizo kutoka Ureno.

XS
SM
MD
LG