Mkazi mmoja anayeishi katika kijiji kilicho karibu na eneo la tukio, alisema baadaye aliona helikopta mbili zikipita na milio ya risasi ikitoka kwao.
"Tuliamshwa na milipuko mikubwa mapema asubuhi. Milipuko hiyo ilikuwa katika kituo cha Umoja wa Afrika. Milio ya risasi ilifuata," mzee wa eneo hilo Mohamed Nur aliiambia Reuters kwa simu kutoka El Baraf, kiasi cha kilomita 130 hadi kaskazini mwa mji mkuu Mogadishu.
Al Shabaab, ambayo imekuwa ikipigana kwa miaka mingi kuiangusha serikali kuu na kusimika utawala wake kwa kuzingatia tafsiri yake kali ya sharia ya Kiislamu, ilidai kuhusika na shambulio hilo.