Mwandishi wa Sauti ya Amerika BMJ Muriithi amepiga picha hizi wakati alipokuwa akiripoti katika kituo cha kupiga kura cha Central Library mjini Arlington, Jimbo la Virginia, akituonyesha mandhari ya kituo cha kupiga kura na jinsi wapigaji kura walivyokuwa wakitekeleza haki yao ya kikatiba kwa utulivu.
Hali ilivyokuwa Jumanne kituo cha kupiga kura Arlington, Virginia siku ya uchaguzi mkuu Marekani
Uchaguzi Marekani wafikia kileleni Jumanne ambapo wananchi wamejitokeza kukamilisha zoezi la kupiga kura katika majimbo mbalimbali, katika uchaguzi utakao amua nani atakuwa rais ajaye wa Marekani.