Duniani leo July 3, 2019
Utawala wa rais Donald Trump, umeachana na mipango yake ya kuweka swali la uraia kwenye sensa ya Marekani ya mwaka ujao. Takriban wahamiaji 40 wengi kutoka Afrika wamekufa na wengine 80 wamejeruhiwa katika shambulizi la anga kwenye kiituo cha wafungwa karibu na mji mkuu wa Libya – Tripoli.