Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 16:45

Zanzibar: Vikao vingi bila suluhisho


Kiongozi wa upinzani Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad
Kiongozi wa upinzani Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad

Imetimia mwezi mmoja kamili tangu kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa Zanzibar, huku viongozi vyama vya CCM na CUF wakiwa na kauli tofauti kuhusiana na hatma ya uchaguzi huo wakatimazungumzo ya kutafuta muafaka yakiendelea kugubikwa na siri nzito kutokana na kutotolewa kwa taarifa yoyote kuhusu mwenendo wa mazungumzo hayo yanayoshirikisha viongozi wakuu akiwemo Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wake wa Kwanza Maalim Seif Sharif Hamad.

Hali ya kisiasa Zanzibar
please wait

No media source currently available

0:00 0:02:21 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Jumla ya vikao vinne tayari vimefanyika katika Ikulu ya Zanzibar na kuwashirikisha viongozi mbalimbali akiwemo Rais Mstaafu wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Rais mstaafu wa Zanzibar Dk.Salmin Amour Juma, Rais mstaafu wa awamu ya sita, Amani Abeid Karume pamoja na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, lakini hakuna taarifa yoyote iliyotolewa hadi hivi sasa.

Wakati mazungumzo hayo yakiendelea katika awamu ya nne, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai amenukuliwa na vyombo vya habari kuwa suala la kurejewa kwa uchaguzi huo halikwepeki, kutokana na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kutangaza rasmi kufuta matokeo hayo katika gazeti la Serikali.

Vuai amenukuliwa akieleza kuwa shabaha ya mazungumzo hayo ni kuendeleza amani pamoja na umoja wa kitaifa kwa wananchi wa Zanzibar, lakini siyo mbadala wa sheria za uendeshaji nchi na wananchi lazima wapatiwe haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi wanaowataka kwa njia ya kidemokrasia.

Hata hivyo, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui ametoa tahadhari kwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuwa endapo itatangaza kurejewa kwa uchaguzi mkuu, mazungumzo hayo hayatakuwa na maana tena ya kuendelea kufanyika, na kusisitiza msimamo wa chama chake kuwa hawako tayari kurejewa kwa uchaguzi huo.

Zanzibar iliingia katika mgogoro wa kisiasa baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Jecha Salim Jecha kufuta matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu, kwa madai ya kugubikwa na kasoro nyingi ikiwemo udanganyifu.

XS
SM
MD
LG