Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 09:38

Wanamgambo wa Nigeria wauwa watu 33


Mabaki ya chuo cha serikali ambapo wanafunzi 60 walichomwa moto hadi kufa Februari 25, 2014
Mabaki ya chuo cha serikali ambapo wanafunzi 60 walichomwa moto hadi kufa Februari 25, 2014

Shambulizi hilo la Alhamis karibu na mpaka wa Cameroon lilifanyika siku moja baada ya mashahidi kuripoti kuwa takribanu wanafunzi 60 waliuwawa katika chuo cha serikali.

Mashahidi na maafisa wa ndani kaskazini mashariki mwa Nigeria wanasema kundi linalotuhumiwa la wanamgambo wa Boko Haram limeuwa watu 33 na kushambulia kwa bomu chuo cha kidini katika jimbo la Adamawa.

Jeshi ambalo mara nyingi haliamini taarifa za idadi ya vifo kutoka kwa mashahidi limesema washambuliaji sita waliuwawa katika tukio hilo pamoja na mwanajeshi mmoja na raia watatu .

Shambulizi hilo la Alhamis karibu na mpaka wa Cameroon lilifanyika siku moja baada ya mashahidi kuripoti kuwa karibu wanafunzi 60 waliuwawa katika chuo cha serikali karibu na jimbo hilo la Adamawa.
XS
SM
MD
LG