Mwakilishi wa Umoja wa Matifa katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, anaemaliza mhula wake anaihimiza serikali ya Kinshasa kuchukua hatua zote muhimu ili kuhakikisha kwamba uchaguzi wa kitaifa unafanyika kwa wakati mwezi ujao na kuwa wa uwazi, wa haki na kujumuisha watu wote.
Alionya kwamba ukiukaji wa haki za binadamu unaongezeka kukiwepo zaidi ya visa 2,200 vya ukiukaji vilivyoripotiwa mwaka huu na kuathiri zaidi ya watu 5000. Amesema vyombo vya serikali vimehusika na nusu ya ukiukaji huo.
Kobler amekua akisimamia kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda Amani huko Congo chenye wanajeshi elfu 22, tangu Agosti 2013.
Mwanadiplomasia huyo ameisihi serikali ya Congo kufanya kazi na Umoja wa Mataifa juu ya mkakati wa kuondoka kwa awamu ya walinda amani nchini humo, akisema “hatuwezi, na haijabidi, kuondoka kwa haraka”.