Alhamisi, Juni 20, 2013 Local time: 01:00

Habari

Rwanda yashutumiwa na UN

Akizungumza katika mkutano mjini nairobi leo , waziri wa mambo ya nje wa Rwanda Louise Mushikawabo amesema nchi yake imeomba ushahidi juu ya tuhuma hizo.

Rais wa Rwanda Paul Kagame
Rais wa Rwanda Paul Kagame
ukubwa wa habari - +

 

Rwanda imejibu ripoti ya wataalamu wa umoja wa mataifa iliyohusisha Kigali na uasi mashariki mwa DRC.

Akizungumza katika mkutano mjini nairobi leo , waziri wa mambo ya nje wa Rwanda Louise Mushikawabo amesema nchi yake imeomba ushahidi juu ya tuhuma hizo.

Amesema nchi yake imetuma barua umoja wa mataifa kutaka maelezo juu ya tuhuma hizo za kulisaidia kundi la M23 nchini DRC. Anasema wamefanya majadiliano ya siku tatu na kundi hilo la wataalamu na kupitia kila tuhuma ambapo wametoa maeleo na nyaraka za uthibitisho za tuhuma za uongo

Waziri huyo amekiri kuwa haamini kama wataalamu wataweza kubadili mawazo yao lakini ilikuwa muhimu kwa Rwanda kujieleza juu ya suala hilo.  
Ameongeza kuwa Rwanda imekosoa kuhusu ushahidi wa ripoti hiyo ya wataalamu wa UN ikiwemo picha za wanajeshi wa M23 waliovalia sare za jeshi la Rwanda. Ripoti hiyo pia imeripoti mazungumzo ya simu baina ya maafisa wa jeshi la Rwanda na wapiganaji wa M23.

Mushikawabo anasema mazungumzo hayo yalifanyika kabla ya uasi kuanza na walikuwa wanajaribu kushawishi wanajeshi kutojitenga.

Baadahi ya wafadhili wa wakubwa wa Rwanda wamejitoa kufuatia ripoti hiyo ya umoja wa mataifa.




mjadala huu umefungwa
Comment Sorting
Maoni
     
Na: W. J. Shadrack Kutoka: Phoenix, AZ
08.08.2012 18:52
Rwanda imekuwa ikikanusha kwa muda mrefu sana kusaidia waasi mashariki mwa Congo. Leo hii wanasema kwamba waliwasiliana na waasi si kwa lengo baya ila kuwashauri wasijitenge kutoka serikalini. Je Rwanda ni nani kwa hawa waasi hadi iwasiliane nao? Kuna siri kubwa sana ambayo Kagame na Museveni wanayo tangu miaka ya themanini.

Mitaani

Loading
12:00:00 / -:--:--