Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 06:03

Mgonjwa wa Ebola kufunguliwa mashtaka Liberia


Hospitali ya Presbyterian iliyoko Dallas, Texas ndipo anapotibiwa mgonjwa wa Ebola, October 1, 2014.
Hospitali ya Presbyterian iliyoko Dallas, Texas ndipo anapotibiwa mgonjwa wa Ebola, October 1, 2014.

Maafisa wa serikali kuu ya Marekani pamoja na wale wa jimbo la Texas wamewawekea karantini watu wanne wa familia ya mtu aliyegunduliwa kuwa na ugonjwa wa Ebola huku maafisa wa Liberia wakisema watamfungulia mashtaka mtu huyo kwa kudanganya kwenye hati za kusafiria katika uwanja wa ndege wa Liberia.

Mgonjwa huyo anayetambuliwa kwa jina la Thomas Duncan raia wa Liberia ni mgonjwa sana lakini anajitambua na ametengwa katika hospitali moja ya Dallas nchini Marekani.

Maafisa wa Liberia wanasema watamfungulia mashtaka Duncan ambaye alipanda ndege kutoka Liberia na kuwasili huko Texas Septemba 20, kwa shutuma za kudanganya kwenye hati za uwanja wa ndege wa Liberia wakati alipoulizwa kama alikuwa na mawasiliano na mtu yeyote aliyekuwa anaugua maradhi ya Ebola.

Hospitali ya Presbyterian
Hospitali ya Presbyterian

Duncan anaripotiwa kujibu ‘hapana’ kwenye swali hilo japokuwa alimsaidia mwanamke mmoja mjamzito aliyekuwa anaugua ugonjwa wa Ebola kuingia katika taxi.

Wakati huo huo nchini Liberia mpiga picha wa Marekani anayefanya kazi na kituo cha televisheni cha NBC News ameambukizwa Ebola. Taarifa zinasema mtu huyo anasafirishwa kurudi Marekani na wafanyakazi wote wanaomsaidia watakua kwenye karantini kwa siku 21.

Shirika la afya duniani-WHO linaripoti kwamba zaidi ya watu 3,000 wamekufa na Zaidi ya 7,000 wameambukizwa ugonjwa huo katika nchi za Guinea, Liberia na Sierra Leone.

XS
SM
MD
LG