Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 19:56

Kanisa Katoliki kujiondoa kwenye uchaguzi Burundi.


 Muandamanaji aficha uso wake kwa majani Burundi.
Muandamanaji aficha uso wake kwa majani Burundi.

Kanisa katoliki la Burundi limesema kuwa linajiondoa katika kuunga mkono uchaguzi unaotarajiwa nchini humo baada ya majuma kadhaa ya michafuko. Kanisa hilo limetoa taarifa Jumanne likisema kuwa limewasihi makisisi wote wanaohudumu kwenye tume za uchaguzi kujiondoa kwenye nyadhifa zao.

Jumatano serikali ya Burundi ilitoa wito kwa wa rundi kutoa michango yao ili kufadhili uchaguzi baada ya wafadhili wa kigeni kutishia kutofadhili iwapo rais Nkurunziza ataendelea na mpango wa kuwania wadhifa kwa muhula wa tatu.

Tangazo la rais mwishoni mwa mwezi uliopita limechochea ghasia na taharuki za kisiasa kwa majuma kadhaa ambapo zaidi ya watu 20 wamekufa na zaidi ya 500 kujeruhiwa kwenye makabiliano na polisi.

XS
SM
MD
LG