Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 11:17

Interpol yafuta vibali vya kuwakamata maafisa wa Rwanda


Nembo ya Interpol
Nembo ya Interpol

Hii ni mara ya pili zikisikika taarifa za kufutwa kwa vibali hivyo. Mara ya kwanza ilikuwa mwezi juni mwaka 2012.

Polisi nchini Rwanda imepokea kwa mikono miwili uamuzi wa polisi ya kimataifa Interpol tawi la Madrid Uhispania wa kufuta kabisa waranti za kuwamakata maafisa wakuu 40 kwenye jeshi la Rwanda.Jaji mmoja nchini Spain alitoa waranti huo mwaka 2008 akiwashutumua mafias hao kutenda makosa ya ukiukaji wa haki za binadamu.

Rwanda Interpol
please wait

No media source currently available

0:00 0:02:05 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Uamuzi wa kufuta kibali cha kukamatwa kwa maafisa hao umekuja miezi michache baada ya mahakama kuu mjini Madrid Uhispania wa kufuta vibali hivyo kwa madai kwamba uchunguzi ulionyesha havina uhalali wa kuendelea kuwepo.

Hii ni mara ya pili zikisikika taarifa za kufutwa kwa vibali hivyo. Mara ya kwanza ilikuwa mwezi juni mwaka 2012.

Miaka mitatu baadaye lakini polisi nchini Uingereza ilimkatamata mkuu wa kitengo cha ujasusi nchini Rwanda liyekuwa amesafiri nchini humo kikazi, suala ambalo lilizusha maandamano makubwa mjini Kigali kupinga kitendo hicho cha polsii ya Uingereza.

XS
SM
MD
LG