Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 00:17

Chama tawala cha Ethiopia kinatarajiwa kupata ushindi katika uchaguzi mkuu


Watu wakisubiri kupiga kura katika jimbo la kaskazini la Tigray, Ethiopia.
Watu wakisubiri kupiga kura katika jimbo la kaskazini la Tigray, Ethiopia.

Vituo vya kupiga kura vilifungwa Jumapili magharibi nchini Ethopia baada ya uchaguzi wa kwanza wa bunge kufanyika tangu kufariki kwa kiongozi wa muda mrefu Meles Zenawi.

Wakosowaji wanasema ni machache yaliyobadilika tangu kufariki kwake na chama chake tawala kinatazamiwa kupata ushindi mkubwa.

Vyama vya upinzani vimelalamika kwamba wafuasi wao wamebughudhiwa na serikali inaendelea kutumia mbinu za ukandamizaji na kuufanya uchaguzi huo kutokua na mana.

Maelfu na maelfu ya wapigajikura walijitokeza tangu alfajiri mjini Addis Abeba na kusimama kwa mistari mirefu katika vituo vya kupiga kura katika shule, ukumbi wa umma na mahema katika mji mkuu wenye wakazi milioni 3 unaokuwa kwa kasi.

Kwa karibu robo karne sasa tangu 1991 chama tawala cha Ethiopia People’s Revolutionary Democratic Front EPRDF kimesimamia mageuzi ya taifa hilo tangu lilipokua chini ya mfumo wa kikomunisti ambapo njaa na umaskini ulikitiri, hadi kugeuka kuwa taifa linalowavutia wawekezaji wa kigeni hii leo.

Kwa hivyo ni wazi mshindi wa uchaguzi wachambuzi wanasema anatazamiwa kuwa ni EPRDF, kwani upinzani hautarajiwi kupata matokeo mazuri, kwani katika uchaguzi wa mwisho wa bunge miaka mitano iliyopita vyama vya upinzani vilipata ushindi wa kiti kimoja bungeni.

Na katika uchaguzi wa 2005 upinzani ulipata viti 147 lakini wengi wa wabunge hao hawakushirikia katika vikao vya bunge wakidai kulikuwa na wizi.

Matokeo ya awali ya uchaguzi wa Jumapili yanatazamiwa mnamo siku chache zijazo huku matokeo rasmi yanatarajiwa kutangazwa mwezi ujao.

XS
SM
MD
LG