Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 20:34

Inawezekana kutokomeza Tumbaku ifikapo mwaka 2040


Zao la Tumbaku
Zao la Tumbaku

Katika mkutano wa dunia wa Tumbaku, na Afya unaofanyika Abu Dhabi, watafiti wanaoongoza katika afya ya jamii wametaka kuuzwa kwa tumbaku kuondolewa kabisa itakapofika mwaka 2040.

Wakiandika katika jarida la utafiti la Uingereza, la The Lancet, watetezi wanasema dunia isiyokuwa na tumbaku ambapo pungufu ya asilimia 5 ya watu wazima wanavuta tumbaku inawezekana chini ya miaka thalathini ijayo.

Katika taarifa mtafiti mwongozaji Robert Beaglehole, kutoka chuo kikuu cha Aauckland, New Zealand, amesema dunia isiyokuwa na tumbaku, kitu kisichofikiriwa na kilichopitwa na wakati ni jambo linalowezekana katika kipindi cha chini ya miaka 30 kutoka sasa.

Lakini hili litawezekana pale tu serekali, na mashirika ya kimataifa kama Umoja wa Mataifa, na WHO, vilevile mashirika ya kiraia yataweka dhamira ya dhati kufikia lengo hilo.

XS
SM
MD
LG