Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 18:56

Ban Ki Moon alaani shambulio la Gaza.


Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon akiongea na waandishi Manhattan, New York June 20, 2014.
Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon akiongea na waandishi Manhattan, New York June 20, 2014.

Baraza la usalama la Umoja wa mataifa lilikutana Jumapili usiku kwa kikao cha dharura juu ya mzozo katika ukanda wa Gaza wakati Israel ikiongeza mashambulizi yake ya anga na nchi kavu.

Jordan iliomba kikao hicho cha dharura baada ya takriban Wapalestina 100 na wanajeshi 13 wa Israel kuripotiwa kuuwawa Jumapili usiku wengi wao katika eneo la Shijaiyah lililoshambuliwa vikali.

Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki Moon anajaribu kutafuta sitisho la mapigano huko Gaza, huku akilaani shambulio la Jumapili na kuomba hatua hiyo ichukuliwe mara moja.

XS
SM
MD
LG