Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 19, 2024 Local time: 13:30

Waliobadili jinsia kutambulika rasmi India.


Watu wa jinsia ya tatu India.
Watu wa jinsia ya tatu India.
Mahakama kuu ya India imeamua kuwatambua rasmi kisheria watu waliobadili jinsia zao na kuwapa haki sawa na kuwatambua kama jinsia ya tatu .

Maamuzi hayo ya kihistoria yanaelekeza serikali kuu na za majimbo kuwajumuisha watu waliobadili jinsia zao katika mipango ya misaada ya serikali kwa watu masikini.

Nyaraka zote rasmi za kikazi zinatakiwa kuwa na kipengele cha watu waliobadili jinsia pamoja na kuwa na mwanamke na mwanaume.

Wanaharakati walisifia maamuzi hayo wakisema yatasaidia kutoa haki sawa kwa kundi ambalo limenyimwa haki katika nchi hiyo.
XS
SM
MD
LG