Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 18:18

Msako unaendelea kwa raia sita wa kigeni waliotekwa Nigeria.


Askari wa Nigeria huko Ibadan.
Askari wa Nigeria huko Ibadan.
Maafisa wa Nigeria wanasema utafutaji unaendelea kwa maharamia wanaodai dola milioni 1.3 kwa raia wa nje sita waliotekwa kutoka kwenye meli Jumapili.
Msemaji wa Polisi huko katika jimbo la Bayelsa amesema Jumatano kuwa mmoja kati ya washukiwa watekaji aliwapigia maafisa kudai malip hayo ili kuwaachia mateka hao.
Amesema watatu kati ya wafanyakazi waliotekwa ni kutoka Ukraine, wawili kutoka India na mmoja kutoka Russia.
Raia hao wa nje walichukuliwa mateka baada ya maharamia kushambulia meli yao kwenye pwani ya Nigeria . Meli hiyo inamilikiwa na Century Group shirika lenye makao yake Nigeria la mafuta .
XS
SM
MD
LG