Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 19:36

Upinzani unasema utashinda uchaguzi Sierra Leone.


Waunga mkono wa chama cha Sierra Leone People's Party (SLPP) wakiandamana kati ya mji wa Freetown na bango la mgombea wao Julius Maada Bio na mgombea mwenza Dr. Kadi Sesay.
Waunga mkono wa chama cha Sierra Leone People's Party (SLPP) wakiandamana kati ya mji wa Freetown na bango la mgombea wao Julius Maada Bio na mgombea mwenza Dr. Kadi Sesay.
Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani huko Sierra Leone, John Benjamin anasema ana imani chama chake kitashinda katika uchaguzi wa rais utakaofanyika Jumamosi, kama ukiwa wa huru na haki.

Katika mahojiano na VOA Benjamin mwenyekiti wa chama cha Sierra Leone Peoples Party, SLPP, anatabiri kwamba wapiga kura watakikimbia chama tawala cha All Peoples Congress kwa sababu ya matatizo ya kiuchumi ya nchi hiyo.

Benjamin pia amesema ana matumaini uchaguzi utakuwa wa huru na haki Amesema ametiwa moyo kutokana na kuwepo kwa wafuatiliaji wa kimataifa ambao wanaweza kufanya kuwa vigumu zaidi kwa mtu yeyote kufanya ghasia wakati wa uchaguzi.

Mgombea wa SLPP Julius Maada Bio ni mmoja kati ya wagombea wanane wanaoshindana na rais aliyeko madarakani Ernest Bai Koroma.
XS
SM
MD
LG