Polisi Afrika Kusini wajitetea kwa kuuwa wachimba migodi
Esther Githui-Ewart
Polisi Afrika Kusini wajitetea kwa kuuwa wachimba migodi
Mwanamke alia baada ya polisi kuuwa wachimba migodi katika mgodi wa Lonmin Platinum Afrika Kusini, Agosti 17, 2012.
Mkuu wa polisi wa Afrika Kusini Riah Phiyenga amesema vikosi vyake viliwafyatulia risasi wafanyakazi wachimba madini wanaogoma kwa ajili ya kujilinda katika ghasia zilizosababisha vifo vya watu 34 na 78 kujeruhiwa.
Kamanda Phiyega amesema polisi walitumia nguvu kupindukia kujilinda wenyewe baada ya kushambuliwa na wachimba migodi wanaogoma waliokuwa na silaha hatari siku ya Alhamis. Kampuni ya mgodi wa Lonmin PLC karibu na Johannesburg, wanakofanya kazi wengi wa wanaogoma imekiri pia kwamba baadhi ya wafanyakazi hao walikuwa na silaha.
Akizungumza na Sauti ya Amerika kutoka Johanesburg mwandishi habari Egbert Mkoko anasema mzozo ulianza wiki moja iliyopita baada ya wachimba madini elfu tatu walipoanza mgomo kudai nyongeza kwa karibu asili mia 300 na hali bora za kazi.
Rais Jacob Zuma alifupisha safari yake ya Maputo na kurudi nyumbani Ijumaa akisema katika taarifa kwamba ameshtushwa na kuchukizwa na kile alichokieleza kuwa ghasia zisizo na maana. Hakusema anayewajibika lakini alivihimiza vyama vya wafanyakazi kufanyakazi na serikali kutanzua hali hiyo.
Polisi wa Afrika Kusini wauwa wachimba migodi 34
1/9An unidentified woman chants as she protests against the police opening fire and killing striking mine workers a day earlier at the Lonmin Platinum Mine near Rustenburg, South Africa, August 17, 2012.
Polisi wa Afrika Kusini wauwa wachimba migodi 34 baada ya kukataa kuondoka kutoka eneo la maandamano
2/9Members of a South African police crime unit investigate the scene of the shooting of miners at the Lonmin mine near Rustenburg, South Africa, August 17, 2012.
Polisi wa Afrika Kusini wauwa wachimba migodi 34 baada ya kukataa kuondoka kutoka eneo la maandamano
3/9An unidentified woman cries as she protests against the police opening fire and killing striking mine workers a day earlier at the Lonmin Platinum Mine near Rustenburg, South Africa, August 17, 2012.
Polisi wa Afrika Kusini wauwa wachimba migodi 34 baada ya kukataa kuondoka kutoka eneo la maandamano
4/9A policeman fires at protesting miners outside a South African mine in Rustenburg, August 16, 2012.
Polisi wa Afrika Kusini wauwa wachimba migodi 34 baada ya kukataa kuondoka kutoka eneo la maandamano
5/9Policemen fire at striking miners outside a South African mine in Rustenburg, August 16, 2012.
Polisi wa Afrika Kusini wauwa wachimba migodi 34 baada ya kukataa kuondoka kutoka eneo la maandamano
6/9A miner runs as police shoot outside a South African mine in Rustenburg, August 16, 2012.
Polisi wa Afrika Kusini wauwa wachimba migodi 34 baada ya kukataa kuondoka kutoka eneo la maandamano
7/9Policemen in teargas and dust open fire on striking miners at the Lonmin Platinum Mine near Rustenburg, South Africa, August 16, 2012.
Polisi wa Afrika Kusini wauwa wachimba migodi 34 baada ya kukataa kuondoka kutoka eneo la maandamano
8/9Police open fire on striking miners at the Lonmin Platinum Mine near Rustenburg, South Africa, August 16, 2012.
Polisi wa Afrika Kusini wauwa wachimba migodi 34 baada ya kukataa kuondoka kutoka eneo la maandamano
9/9A paramedic (front L) receives help from a policewomen as he tends to the injured after protesting miners were shot outside a South African mine in Rustenburg, August 16, 2012.
Polisi wa Afrika Kusini wauwa wachimba migodi 34 baada ya kukataa kuondoka kutoka eneo la maandamano
Previous slide
Next slide
Msemaji wa chama cha kitaifa cha wachimba madini Lesina Seshoka anasema sehemu ya mvutano huo imechochewa na uwamuzi wa wafanyakazi kuanza mgomo bila ya kupata uungaji mkono wa chama cha wafanyakazi.