Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 21:22

Klabu ya waandishi wa habari Iringa yasitisha ushirikiano na polisi.


Mmoja wa makamishna wa jeshi la polisi nchini Tanzania.
Mmoja wa makamishna wa jeshi la polisi nchini Tanzania.
Klabu ya waandishi wa habari mkoani Iringa –IPC nchini Tanzania, kwa kushirikiana na waandishi wote wanaofanya kazi mkoani humo, kuanzia Jumanne imetangaza kusitisha ushirikiano wa kikazi baina yao na jeshi la polisi mpaka pale taarifa au majibu sahihi kutoka vyombo huru zitakapotolewa kujua aliyemuuwa mwandishi wenzao Daudi Mwangosi wakati wa vurugu za chama cha demokrasia na maendeleo -Chadema na polisi.

Kazi hizo ni pamoja na kuwataarifu waandishi wote kuacha kwenda katika ofisi ya kamanda wa polisi kupata taarifa za matukio mbalimbali .

Mwangosi ambaye pia ni mwandishi wa habari wa Chanel Ten alifariki Jumatatu majira ya saa 10 jioni baada ya kupigwa na kile kinachosadikiwa kuwa bomu katika vurugu za wafuasi wa Chadema waliokuwa wakitawanywa na polisi.

Kumezuka utata wa nani anahusika na tukio hilo huku jeshi la polisi likitoa taarifa jumanne kusema uchunguzi wake unaonesha kuwa bomu lililompiga mwandishi Mwangosi lilitoka upande wa Chadema.
XS
SM
MD
LG