Viongozi wa Ulaya wako katika siku ya pili ya mkutano hivi leo wa Baraza la EU mjini Brussels, ambapo mazungumzo hivi leo yanalenga jinsi ya kuondoa tatizo la kushuka kwa uchumi katika umoja huo na kuuzuia kuwa nyuma zaida ya China na Marekani.
Pentagon imesema Lloyd Austin na Admirali Dong Jun wa China walijadili uhusiano wa ulinzi na masuala ya usalama wa kimataifa
Boti ilikuwa imebeba jumla ya watu 12 wengi wao wakiwa wakulima msimamizi wa wilaya ya Caia aliliambia shirika la habari la AFP.
Waziri wa mambo ya nje wa Israel amesema amewasiliana na mataifa zaidi ya 30 kushinikiza vikwazo dhidi ya mpango wa makombora wa Iran.
Mvua ilianza usiku kucha na kuvuruga safari za ndege katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dubai
Wizara ya biashara ya Marekani Jumatatu imetoa mkopo wa dola bilioni 6.4 kwa kampuni ya elektroniki ya Samsung yenye makao yake Korea Kusini, ili kujenga kiwanda chake kipya cha kutengeneza chip za komputa mjini Taylor, Texas pamoja na kupanua kiwanda cha zamani mjini Austin kwenye jimbo hilo hilo.
Shirika lisilotafuta faida linasaidia wahamiaji kupata mafunzo kuhus ajira. Mafunzo haya hutolewa kuwaandaa wafanyakazi kufahamu masuala ya usalama katika viwanja vya ujenzi. Hii ni hatua ya kukabiliana na uhaba wa wafanyakazi wa ujenzi katika jiji la New York. Endelea kusikiliza...
Kesi ya kwanza ya uhalifu inayomkabili Rais wa zamani wa Marekani inatarajiwa kuanza wiki hii huko New York.
Israel, Jumapili imesema Iran ilifanya mashambulizi ya makombora 320 ya kivita dhidi yake katika shambulio ambalo halijawahi kushuhudiwa, lakini ulinzi wake wa anga pamoja na Marekani na nchi nyingine zinazoiunga mkono uliyatungua kwa asilimia 99.
Msemaji wa masuala ya usalama wa taifa wa White House, John Kirby, amesema Marekani na washirika wengine wanaona yalikuwa ni mafanikio ya makubwa ya kijeshi ya Israel, katika kuzima mashambulizi ya zaidi ya ndege zisizo na rubani 300 na makombora yaliyorushwa na Iran.
Donald Trump, anaelekea mahakamani Jumatatu, akiwa ni rais wa kwanza mstaafu wa Marekani kukabiliwa na mashtaka ya uhalifu na tishio la kufungwa jela iwapo atapatikana na hatia.
Nyota wa zamani wa Ligi ya Mpira wa Marekani NFL na mcheza filamu ambaye alifutiwa mashtaka ya mauaji ya mkewe na rafiki yake wa kiume katika kesi iliyoteka Marekani na dunia amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 76.
Pandisha zaidi