Zimbabwe imefikia makubaliano ya kuuza almasi zake zilizochimbwa katika mgodi wenye mzozo wa Marange.
Baraza la almasi duniani lilisema makubaliano hayo yalifikiwa jumanne kwenye mkutano katika mji mkuu wa Congo Kinshasa. Iliidhinishwa na wanachama wa Kimberly Process mpango uliowekwa kuzuia kile kilichoitwa almasi za damu kufikia masoko ya kimataifa .
Makubaliano hayo yanaruhusu migodi miwili ya Marange kuuza almasi kwenye soko la kimataifa. Mgodi wa tatu ulioendeshwa na kampuni ya wachina ya Angin , utaruhusiwa kuanza tena mauzo kufuatia kupitishwa na wasimamizi wa Kimberly.