Wazazi wa wasichana wa shule waliotekwa nyara na kundi la Boko Haram wamesema wanangoja kusafiri kuelekea Cameroon ili kuthibitisha iwapo msichana aliyetaka kujitoa muhanga aliyekamatwa na kutoka Chibok kaskazini mashariki mwa Nigeria ambapo wasichana 276 wa shule walitekwa karibu miaka miwili iliopita ni miongoni mwao.
Hata hivyo mvutano umeibuka kwa kuwa mtoto aliekamatwa Ijumaa akiwa na mkanda wenye vilipuzi anaonekana kuwa na umri wa takriban miaka 10. Mzazi Yakubu Nkeki kutoka Chibok amesema anaweza kudhibitisha iwapo atamuona msichana huyo.