Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 19, 2024 Local time: 10:32

Kura za wahamiaji zina umuhimu katika uchaguzi wa rais Marekani


Wafuasi wa mageuzi ya uhamiaji walikusanyika kwenye chuo kikuu cha Colorado kuzindua kampeni ya "Nchi yangu, kura yangu," Oktoba 2015.
Wafuasi wa mageuzi ya uhamiaji walikusanyika kwenye chuo kikuu cha Colorado kuzindua kampeni ya "Nchi yangu, kura yangu," Oktoba 2015.

Inakadiriwa takriban waislamu milioni 3.5 wanaishi hapa Marekani, ikiwa ni theluthi moja ya wamarekani wenye asili ya kiafrika, waislamu hao wengi wao ni wahamiaji kutoka dazeni ya nchi za asia, afrika na mashariki ya kati.

Kwasababu wahamiaji wengi wa kiislamu wanatokea kwenye nchi zenye demokrasia ndogo ya uchaguzi na viwango vya chini vya kujihusisha kijamii, hawakuwa na kawaida ya kupiga kura kwa idadi kubwa. Lakini hilo limebadilika tangu mwaka 2000 pale wamarekani waislamu, waliposhawishiwa na taasisi za kijamii kujitokeza kwa wingi na kumuunga mkono mgombea wa chama cha Republican, George W. Bush.

please wait

No media source currently available

0:00 0:07:59 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Mwaka 2003, Zaidi ya asilimia 90 ya wamarekani waislamu walimpigia kura mgombea wa chama cha Democratic, John Kerry wakati ambapo mwaka 2008 na 2012 walimpigia kura Barack Obama mdemocrat mwingine aliyekuwa anawania urais.

Na swala jingine katika uchaguzi wa mwaka ni uandikishaji na kuhamasisha wapiga kura, watu wanaojitolea katika vyama viwili vikuu vya siasa pamoja na asasi nyingine wamekuwa wakitembea nyumba kwa nyumba katika jimbo muhimu sana la uchaguzi la Ohio ili kupata idadi kubwa ya wahamiaji kushiriki katika uchaguzi wa mwaka huu. Jamii zinazotupiwa jicho ni pamoja na zile za wahamiaji kutoka Asia, Afrika na Mashariki ya Kati.

XS
SM
MD
LG