Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 04:37

Wapiganaji wa Taliban wamethibitisha kupeleka ujumbe mkali Islamabad


Wanamgambo wa Taliban huko Pakistan
Wanamgambo wa Taliban huko Pakistan

Wapiganaji wa Taliban nchini Afghanistan wamethibitisha kupeleka ujumbe wa hali ya juu huko Islamabad kwa mazungumzo na maafisa wa Pakistan wakisema wana matumaini kwamba ziara hiyo itakuwa na matokeo mazuri kwa maslahi ya nchi zote mbili.

Msemaji wa kundi hilo la wanamgambo wa kiislam ameiambia VOA Jumatano kwamba ujumbe wa Taliban umesafiri kutoka makao yake makuu ya kisiasa huko Qatar kufanya mazungumzo katika masuala ya ya uhusiano wa karibu na shughuli za kibiashara na mpajkani kati ya nchi hizo mbili jirani.

Maafisa wa Pakistan bado hawajathibitisha juu ya kuwepo na sababu ya ziara ya Taliban.

XS
SM
MD
LG