Kundi la wanawake kutoka makabila mbali mbali eneo la Kivu kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC yalianza kampeni kwa makundi ya wapiganaji kwenye eneo hilo kuweka silaha zao chini na kufanya maridhiano ya kuleta amani miongoni mwa makabila hayo.
Mwandishi wa Sauti ya Amerika-VOA katika eneo la Kivu kaskazini aliripoti kwamba kila kabila huko limekuwa na kundi lake kama walinzi na hiyo inaonekana kuwa chanzo cha vita vinavyotokea huko mara kwa mara.