Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 12:01

Upinazi unadai wizi wa kura huko Uganda


Kiongozi wa upinzani Kizza Besigye akizungumza kwenye mkutano wa hadhara Kampala.
Kiongozi wa upinzani Kizza Besigye akizungumza kwenye mkutano wa hadhara Kampala.

Uchaguzi Uganda wagubikwa na madai ya rushwa

Waganda wamepiga kura Ijumaa katika uchaguzi unaotegemewa kumpa rais Yoweri Museveni muhula wa nne madarakani ambao tayari umegubikwa na madai ya rushwa.

Muhula mpya utafanya muda wa Bw. Museveni madarakani kufikia miaka 30. Lakini pengine rais huyo anakumbana na uchaguzi mgumu kuliko yote katika miaka 25 wakati daktari wake wa zamani Kizza Besigye akimpinga kwa mara ya tatu mfulululizo.

Bw. Besigye anayeongoza muungano wa upinzani wa vyama vinne ameishutumu serikali kwa kujaribu kuiba kura, rais Museveni anapinga madai hayo.

XS
SM
MD
LG