Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 23:09

VOA yamuenzi Mngodo


Picha ya aliyekuwa mtangazaji wa VOA Gdfrey Mngodo.
Picha ya aliyekuwa mtangazaji wa VOA Gdfrey Mngodo.

Godfrey Mngodo alikuwa mtangazaji wa kwanza wa idhaa ya Kiswahili ya sauti ya Amerika ilipoanzishwa mwaka 1962 .

Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika inamkumbuka aliyewahi kuwa mtangazji wake Mzee Godfrey Mngodo aliyefariki dunia Ijumaa Septemba 11.

Godfrey Mngodo alikuwa mtangazaji wa kwanza wa idhaa ya Kiswahili ya sauti ya Amerika ilipoanzishwa mwaka 1962 .

Kwa mujibu wa taarifa za mtoto wa marehemu, Kinyemi Mngodo, Marehemu Mzee Godfrey Mngodo amefariki katika hospitali ya Dar Group jijini Dar es salaam baada ya kuugua kwa muda maradhi ya figo.

Taratibu za mazishi zinafanyika nyumbani kwa mtoto wa marehemu Yombo Vituka jijini Dar es salaam lakini taarifa za awali zinaeleza kuwa marehemu anatarajiwa kuzikwa kijijini kwake Muheza mkoani Tanga.

Mzee Godfrey Mngodo aliyezaliwa Februari 7 mwaka 1939 pia alikuwa miongoni mwa watangazaji wa mwanzo wa iliyokuwa Tanganyika Broadcasting Corporation kabla ya kubadilishwa na kuwa Redio Tanzania Dar es salaam.

Atakumbukwa pia kama mwanzilishi wa chumba cha habari mara kilipoanzishwa kituo cha utangazaji cha Dar es salaam Televisheni , DTV mwaka 1994 na aliendelea kutumikia kituo hicho baada ya kuanzishwa pia kituo cha CHANNEL TEN kama Msimamizi wa habari na baadaye Meneja rasilimali watu mpaka alipostaafu mwishoni mwa mwaka 2008.

Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika inatoa pole kwa ndugu na jamaa na Marafiki wa Marehemu Godfrey Mngodo.

XS
SM
MD
LG