Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 24, 2024 Local time: 21:06

UN: Maovu ya ISIS yafikia ngazi nyingine


Displaced people from the minority Yazidi sect, fleeing violence from forces loyal to the Islamic State.
Displaced people from the minority Yazidi sect, fleeing violence from forces loyal to the Islamic State.

Wachunguzi wa Umoja wa Mataifa wanasema kampeni ya kupangwa ya ubakaji, utumwa na mauaji inayofanywa na kundi la wanamgambo wa Islamic State dhidi ya 'Yazidis' inafikia kiwango cha mauaji ya halaiki, uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu.

Bones, suspected to belong to members of Iraq's Yazidi community, are seen in a mass grave on the outskirts of the town of Sinjar, November 30, 2015.
Bones, suspected to belong to members of Iraq's Yazidi community, are seen in a mass grave on the outskirts of the town of Sinjar, November 30, 2015.

Tume ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Syria imetoa ripoti yake mapema leo ikieleza kwa kina kampeni ya makusudi ya Islamic State ya kutokomeza wakazi wa Ki-Yazidi wanaopatikana katika wilaya ya Sinjar, nchini Iraq pekee yake.

Kamishna Paulo Pinheiro amesema "mauaji ya halaiki yametokea na yanaendelea na Islamic State inahusika katika kila kukamatwa kwa wanawake, watoto ama wanaume wa Yazidi ambaye wamekamatwa na kufanyiwa ukatili mkubwa."

XS
SM
MD
LG