Vijana barani Afrika wamehimizwa kutumia mitandao ya kijamii kujinufaisha na wala sio katika mambo yasiyokuwa na faida.
Ujumbe huu umetolewa kwa vijana nchini Kenya baada ya kuwasili kwa kundi la vijana kutoka Afrika kusini chini ya mradi wa building bridges kuangazia miradi kadhaa ya vijana wa Kenya na kunakili changamoto zao kabla ya kongamano la vijana kuandaliwa jijini Nairobi mwaka huu.
Itakumbukwa kuwa shutuma nyingi zidi ya matumizi mabaya ya mitandaoni zimetolewa katika maeneo mengi duniani. Mwandishi wa Voa Swahili mjini Nairobi Liberty Adede ameandaa taarifa hii.