Shirika la maendeleo la USAID lenye makao yake nchini Marekani linatoa msaada wa maji safi kwa wakaazi wa maeneo ya mashambani katika mpaka wa Uganda na Kenya wa Busia kwa kujenga na kukarabati matenki ya maji safi.
Hatua hii imefuata baada ya Sauti ya Amerika-VOA kuangazia matatizo ya wakaazi wa maeneo hayo ya kukosa maji safi na kutegemea maji ya mtoni hasa msimu wa majira ya kiangazi.
Mwandishi wetu wa Kampala Kennes Bwire anaripoti.