Waziri wa mambo ya nje wa Burundi Jumatatu amekanusha kuwa nchi hiyo iko katika hali mbaya ya ghasia na badala yake amesema kuna maelezo tofauti yanayotolewa na makundi yenye misimamo mikali na baadhi ya vyombo vya habari.
Katika kikao kilichofanyika Jumatatu na kuhuduriwa na wawakilishi nmbalimbali wengi wameshutumu ghasia zinazoendelea hadi sasa tangu zilipochochewa wakati wa uchaguzi mkuu nchini humo.