Wapiga kura nchini Uganda wanatarajia kushuhudia wagombezi wote wa urais wakijadili maswala yanayowahusu katika mjadala utaopeperushwa moja kwa moja na vyombo vya habari Ijumaa jioni.
Japo matayarisho yamekamilika na wageni waalikwa wameanza kufika kwenye ukumbi wa mjadala, ushiriki wa rais wa sasa Yoweri Museveni bado haujulikani huku waandalizi wakiwa na kibarua kigumu kumshawishi Dkt Kiiza Besigye kushiriki.
Mwandishi wetu wa Kampala Kennes Bwire anaripoti.