Ripoti ya shirika la kutetea haki za binadamu (HRW) imeeleza Jumatatu kwamba vyombo vya habari nchini Uganda vinakandamizwa wakati nchi hiyo ikijiandaa na uchaguzi mkuu Febrauri 18 mwaka huu .
Kwa mujibu wa mchambuzi Akol Amazima akizungumza na Sauti ya Amerika anasema joto la kisiasa likipanda wahariri wengi vibarua vyao vinakuwa matatani kwani wanakuwa wakipokea vitisho vya hapa na pale.
Vile vile akitaja waandishi wa habari waliopata matatizo akitolea mfano mwandishi wa WBS ambaye zaidi ya miezi 6 yuko hospitali kwa kushambuliwa , hali kadhalika mwanahabari wa NTV alivunjiwa kamera yake akizuiwa asipige picha mkutano wa Dk.Kiza Besigye.