Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 18:58

Uturuki yafungua Ubalozi Kigali


Kigali, Rwanda
Kigali, Rwanda

Kwa mara ya kwanza, Uturuki imefungua ubalozi wake mjini Kigali.Serikali ya Rwanda imekaribisha uamuzi huo wa Uturuki na kusema kuwa unaondoa adha iliyokuwepo ambapo wananchi wa Rwanda waliotaka kusafiri Uturuki walilazimika kwenda Kampala, Uganda kuomba visa ya kusafiria.

please wait

No media source currently available

0:00 0:02:11 0:00
Kiungo cha moja kwa moja


Uamuzi huo umefuatia ule wa Rwanda wa kufungua ubalozi wake mjini Ankara Uturuki miaka 4 iliyopita. Nchi zote mbili zimesaini mikataba mbali mbali ya ushirikiano na maendeleo .

Waziri wa mashauri ya kigeni wa Uturuki amesema mikataba hiyo inalenga kuinua kiwango cha uwekezaji baina ya mataifa yote mawili. Kama anvyosimulia Sylvanus Karemera kutoka Kigali.

XS
SM
MD
LG