Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 01:28

Sudan na Chad zamtafuta mhandisi wa China aliyepotea .


Ramani ya Sudan
Ramani ya Sudan

Wanajeshi kutoka Sudan na Chad wanamtafuta mhandisi wa China aliyepotea . Msemaji wa jeshi la sudan alisema leo kwamba maafisa wana taarifa kuwa mhandisi huyo alishikiliwa mateka huko Chad.

Sudan na Chad zamtafuta mhandisi wa China aliyepotea.

Wanajeshi kutoka Sudan na Chad wanamtafuta mhandisi wa China aliyepotea .

Msemaji wa jeshi la sudan alisema leo kwamba maafisa wana taarifa kuwa mhandisi huyo alishikiliwa mateka huko Chad.

Shirika la habari la Ufaransa liliripoti kuwa raia huyo wa China yuko Chad akifanya kazi kwenye mradi wa kusambaza maji kwenye mji mmoja.

Maafisa hawajasema kama kuna madai yoyote ya fidia yaliyotolewa.

Mwezi uliopita rubani watatu wa ndege walitekwa katika jimbo la Darfur wakitishiwa na bunguki na kushikiliwa kwa siku mbili .

XS
SM
MD
LG